(Translated by https://www.hiragana.jp/)
Retisi - Wikipedia, kamusi elezo huru

Retisi (pia: Reticius, Rheticius, Rheticus, Rhétice; alifariki 320 hivi) kwa miaka 25 hivi alikuwa askofu wa Autun, leo nchini Ufaransa, akiwa wa kwanza kati ya wanaojulikana [1][2].

Kwa agizo la kaisari Konstantino Mkuu alishiriki sinodi mbili zilizojaribu kumaliza farakano la Donato lilitokea Afrika Kaskazini[3].

Gregori wa Tours alimsifu katika maandishi yake [3] na Jeromu alimtaja pamoja na vitabu viwili alivyoviandika[4].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 15 Mei[5].

Tazama pia

hariri

Tanbihi

hariri
  1. "Autun". Catholic Encyclopedia. 2009. Iliwekwa mnamo Aprili 23, 2009.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  2. http://www.santiebeati.it/dettaglio/65490
  3. 3.0 3.1 "Reticius von Autun". Ökumenisches Heiligenlexikon. Iliwekwa mnamo Aprili 23, 2009.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  4. Reticius, bishop of Autun, among the Aedui, had a great reputation in Gaul in the reign of Constantine. I have read his commentaries On the Song of Songs and another great volume Against Novatian but besides these, I have found no works of his. Cfr. Saint Jerome. "Lives of Illustrious Men. Chapter LXXXII". Christian Classics Ethereal Library. Iliwekwa mnamo Aprili 23, 2009.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  5. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje

hariri
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.