(Translated by https://www.hiragana.jp/)
Lango:Afrika - Wikipedia, kamusi elezo huru Nenda kwa yaliyomo

Lango:Afrika

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Milango ya Wikipedia: Sanaa · Utamaduni · Jiografia · Afya · Historia · Hisabati · Sayansi · Falsafa · Dini · Jamii · Teknolojia

hariri  fuatilia  

Lango la Afrika

Afrika ni bara la pili duniani kwa ukubwa, likiwa na eneo la kilometa za mraba zipatazo 30,370,000 na kwa idadi ya wakazi, hao wakiwa 1,225,080,510 (mwaka 2016). Asia ndiyo bara pekee la kushinda Afrika.

Neno "Afrika" limetokana na lugha ya Kilatini ya Roma ya Kale. Waroma kwa jina hilo hawakumaanisha bara lote bali eneo katika Tunisia ya leo tu. Asili yake ni kabila la "Afrig" lililoishi sehemu zile. Wakati huo Wagiriki wa Kale walitumia zaidi jina la Libya kwa ajili ya nchi kusini kwa Bahari ya Mediteraneo. Maeneo ya ndani kuelekea kusini mara nyingi yaliitwa kwa jina la "Ethiopia" linalomaanisha nchi ya watu weusiweusi (kwa Kigiriki "aithiops": aliyechomwa na jua).

hariri  fuatilia  

Nchi za Afrika

hariri  fuatilia  

Jamii

hariri  fuatilia  

Wasifu Uliochaguliwa

Amiri Muammar al-Gaddafi (Kiarabu:معمر القذافي Mu‘ammar al-Qadhāfī) ni kiongozi wa taifa la Libya. Amezaliwa katika familia ya mabedawi (wafugaji wahamiaji) mnamo mwaka 1942. Baada ya masomo ya sheria kwenye chuo kikuu cha Libya alijiunga na jeshi 1963 akasoma kwenye chuo cha kijeshi cha Sandhurst (Uingereza) 1965. 1 Septemba 1969 pamoja na maafisa wenzake alipindua serikali ya mfalme Idris I na kutangaza Jamhuri ya Kiarabu ya Libya. Ingawa hana cheo rasmi anaendelea kutawala nchi yake akiitwa "Kiongozi wa mapinduzi ya 1 Septemba ya Jamahiriya ya Ujamaa ya watu ya Kilibya-Kiarabu".


hariri  fuatilia  

Makala iliyochaguliwa

Hifadhi ya Taifa ya Hell's Gate iko kusini mwa Ziwa Naivasha nchini Kenya, kaskazini magharibi mwa Nairobi. Mbuga ya Taifa ya Hell's Gate inapata jina lake kutokana na vifusi vyembamba vilivyovunjika kutoka kwa miinuko, kwa wakati mmoja ilikuwa vijito vya ziwa la kale lililolisha binadamu wa kwanza katika Bonde la Ufa. Ilianzishwa mwaka wa 1984. Mbuga hii ndogo inajulikana kwa wingi wake wa aina ya wanyamapori na kwa ajili mandhari yake. Hii ni pamoja na minara ya Fischer's Tower na Central Tower na Giba ya Hell's Gate. Hifadhi hii ya Taifa pia ni makao ya vituo vitatu vya nishati za mvuke zilizoko Olkaria. Hifadhi hii ina kambi tatu msingi na inajumuisha a Kituo cha Utamaduni wa Wamasai, kinachotoa elimu kuhusu kabila la Kimasai utamaduni na mila zake. Hell's Gate National Park ilipata jina lake kutokana na kuvunjika kwembamba kwa miamba yake, ambayo kwa wakati mmoja ilikuwa vijito vya ziwa la kale lililolisha binadamu wa awali katika Bonde la Ufa. Ilipokea jina la "Hell's Gate" kutoka kwa Wapelelezi Fisher na Thomson mwaka wa 1883.


hariri  fuatilia  

Picha Iliyochaguliwa

hariri  fuatilia  

Je, wajua...?

...kwamba Milima ya Udzungwa ni jina la hifadhi inayopatikana katika nchi ya Tanzania na jina hili limetookana na milima hiyo ya udzungwa ambayo ndani yake ni makazi ya wanyama pori wa aina mbalimbali.

hariri  fuatilia  

Masharika ya Wikimedia